Mzuka wa siasa unazidi kuwapanda wasanii wengi wa Bongo Flava. Hata
hivyo Baba Levo hautaki ubunge bali ametangaza nia ya kugombea udiwani
kupitia chama cha ACT – Tanzania katika kata ya Mwanga Kaskazini mkoani
Kigoma.
Akizungumza na 255 ya XXL ndani ya Clouds FM, Baba Levo alisema anajipanga kuanzisha kitu kinachoitwa mgodi wa diwani.
“Ndani ya mgodi wa diwani kutakuwa na timu ya mpira, timu ya
kuogelea, kutakuwa na timu ya mabondia, timu ya bongo movie na timu ya
wanamuziki,” alisema.
“Ndani ya mgodi kutakuwa na watu kama 200, baada ya kuwa na watu mia
mbili, kwa sababu mimi ndo nitakuwa diwani na nitakuwa najua ni fungu
gani limetoka kwaajili ya watu wa Mwanga Kaskazini, kwajili ya miradi
mbalimbali yaani kazi zote zitakazohusu Mwanga Kaskazini, zitafanywa na
timu ambayo ninayo mimi yaani Mgodi wa diwani. Yaani deal zote
zinazokuja tutazifanya sisi,” aliongeza rapper huyo.

Note: Only a member of this blog may post a comment.