Rest in peace! Mwanamke, Glorian Zuberi ‘Fatuma’ amefariki dunia
baada ya bodaboda aliyokuwa amepanda kugongwa na gari aina fuso,
akitokea kujirusha.
Tukio
hilo la kusikitisha lilijiri hivi karibuni, majira ya saa 8:00 usiku
katika Barabara Kuu ya Morogoro-lringa eneo la Kwajeta jirani na Ukumbi
wa Contena mjini hapa.
Habari zilieleza kwamba mwanamke huyo alipokuwa kwenye ukumbi huo
akila bata, alionekana kuwa kinara kwa kukata nyonga kila muziki wa
sebene uliposikika huku waimbaji wa bendi iliyokuwa ikipiga ‘laivu’
wakilirusha jina lake kila aliponyanyuka kucheza.
Ilidaiwa kwamba, mishale ya saa nane kasoro usiku, aliamua kutoka
ukumbini hapo akiwa na mwanaume aliyedaiwa ni mchepuko na kukodi
bodaboda kisha kupakizana ‘mshikaki’.
Dakika tano baadaye, kiongozi wa bendi hiyo ya Maisha Mapya, Joshua
Malekela alitangaza: ”Jamani hatuwezi kuendelea kupiga muziki, yule
Fatuma aliyekuwa akicheza sebene amefariki dunia na watu wengine wawili
baada ya bodoboda waliyokuwa wamepanda kugongwa na fuso.”
Baada
ya taarifa hizo, mashabiki na mwandishi wetu aliyekuwa akisaka matukio,
walifika eneo la tukio na kumshuhudi Fatuma, mwanaume aliyekuwa naye na
dereva wa bodaboda wakiwa katikati ya barabara wamefariki dunia huku
miili yao ikiwa imeharibika.
”Kuna fuso lilikuwa likitokea Msamvu lilikuwa spidi kuelekea lringa
ndipo dereva wa bodaboda aliyekuwa amepakia mshikaki alikata kona mbele
ya fuso bila kuangalia nyuma wala kutoa ishara ndipo fuso likawagonga
kwa nyuma na halikusimama,’’ alisema Juma Hamis, mmoja wa mashuhuda wa
tukio hilo.
Akizungumza
na Ijumaa Wikienda, mama ma mzazi wa Fatuma, Etrapia Clemens alisema
kuwa, siku ya tukio mwanaye alimuaga anakwenda ‘kupoteza mawazo’ kwenye
Ukumbi wa Contena na wakati akireja nyumbani alipata ajali na kufa
papohapo.
Alisema miezi kadhaa iliyopita mwanaye alibadili dini na kufunga ndoa
ya Kikristo na mumewe, William Mwalubuch ambaye wakati mkewe anakutana
na umauti alikuwa safarini jijini Dar.
Marehemu Fatuma alizikwa katika Makaburi ya Wakristo ya Kolla mjini hapa.

Note: Only a member of this blog may post a comment.