Akihutubia mamia ya wananchi katika
mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma
jana baada ya kupitishwa na CCM kuwania urais, Dk. Magufuli alitangaza
vita ya kupambana na wazembe, mafisadi, wala rushwa na wabadhirifu kuwa
atapambana nao kwa nguvu zake zote.
Dk. Magufuli alisema: “Wazembe na wabadhirifu watakaokuwa pamoja na wezi na wala rushwa nitawashughulikia kwa upole sana. Nitalinda uhuru wa mipaka yetu kwa kuwa ni ya watu wote ingawa nita-deal na mtu atakayehatarisha uhuru wetu…Watanzania najua wana matumaini makubwa na mimi.”
Aidha, mgombea huyo aliwaeleza wakazi wa Dodoma kuwa iwapo atapewa ridhaa na Watanzania kuwa Rais wa Tanzania atahahikisha vijana wanatatuliwa changamoto za ajira kwa haraka na kwa kasi zaidi.
Dk. Magufuli alisema: “Wazembe na wabadhirifu watakaokuwa pamoja na wezi na wala rushwa nitawashughulikia kwa upole sana. Nitalinda uhuru wa mipaka yetu kwa kuwa ni ya watu wote ingawa nita-deal na mtu atakayehatarisha uhuru wetu…Watanzania najua wana matumaini makubwa na mimi.”
Aidha, mgombea huyo aliwaeleza wakazi wa Dodoma kuwa iwapo atapewa ridhaa na Watanzania kuwa Rais wa Tanzania atahahikisha vijana wanatatuliwa changamoto za ajira kwa haraka na kwa kasi zaidi.
“Nataka
niwahakikishie Watanzania na wana -CCM kwa ujumla kwamba CCM ipo tayari
kwa mageuzi ya uhakika na ya haraka kwa watu wote. Sitawaangusha
Watanzania na vyama vingine vyenye itikadi tofauti na Chama cha
Mapinduzi,” alisema na kushangiliwa na wananchi waliohudhuria mkutano huo.
Aliwapa matumaini wanachama waa chama hicho kwamba hatawaangusha kwani dhamana aliyopewa ni kubwa hivyo atahakikisha CCM inapata ushindi mkubwa wakati wa uchaguzi mkuu.
Aliwapa matumaini wanachama waa chama hicho kwamba hatawaangusha kwani dhamana aliyopewa ni kubwa hivyo atahakikisha CCM inapata ushindi mkubwa wakati wa uchaguzi mkuu.
“Leo
ni siku muhimu katika chama chetu, hata kwangu mimi mwenyewe… naona ni
siku muhimu. Sitawaangusha Oktoba..narudia tena sitawaangusha…hata wale
wa vyama vingine sitawaangusha, ” alisema na kuongeza.”
“Nitatekeleza mambo yote yaliyomo ndani ya ilani ya uchaguzi kuhusu masuala ya barabara, viwanja vya ndege, maji, umeme na mengine nitahitaji sana msaada kutoka kwenu.”
“Nitatekeleza mambo yote yaliyomo ndani ya ilani ya uchaguzi kuhusu masuala ya barabara, viwanja vya ndege, maji, umeme na mengine nitahitaji sana msaada kutoka kwenu.”
Dk. Magufuli katika mkutano huo
alitambulishwa na Rais Jakaya Kikwete, muda mfupi baada ya kutangazwa
matokeo yaliyompa ushindi wa kupeperusha benderea ya CCM wakati wa
uchaguzi mkuu dhidi ya vyama vya upinzani.
Baada ya kuchaguliwa na Mkutano Mkuu wa CCM kuwa mgombea urais wa chama hicho, Dk. Magufuli alimteua Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulikia mambo ya Muungano, Samia Hassan Suluhu kuwa mgombea wake mwenza.
Baada ya kuchaguliwa na Mkutano Mkuu wa CCM kuwa mgombea urais wa chama hicho, Dk. Magufuli alimteua Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulikia mambo ya Muungano, Samia Hassan Suluhu kuwa mgombea wake mwenza.


Note: Only a member of this blog may post a comment.