Monday, July 13, 2015

Anonymous

DUNIA IMEKWISHA! Kijana Akutwa akimnajisi Bata Huko Bukombe!

Wananchi wa kitongoji cha Bomani wamemkamata kijana mwenye miaka 28 anayedaiwa kukutwa akimnajisi bata.

Shuhuda wa tukio hilo Sacina Nangere alisema akiwa na wenzake walisikia kelele za bata nyuma ya nyumba kwa muda mrefu na kuamua kukimbia kuangalia kuna nini, na alipofika alimkuta mtuhumiwa huyo akifanya kitendo hicho. 

“Nilirudi kukimbia kumwita mama akaone na alipofika huyo jamaa alimtupa bata na kukimbilia kwa jirani alikokua amefikia”.

Mmiliki wa bata huyo Susana alisema akiwa jikoni akiandaa chakula mtoto wake alimwita na kumwambia akaone mgeni wa jirani yake anachomfanyia bata wao. 

“Sikuamini macho yangu hadi anamtupa bata na kuondoka, tulipiga yowe na wananchi wakanisaidia kumkamata wakati akijaribu kutoroka”. 

Balozi wa nyumba 1o alisema mama huyo alifika nyumbani kwake akiwa na bata aliyenajisiwa huku akiomba msaada na alipoangaliwa alikutwa kweli ameharibiwa na kijana huyo. 

Kamanda wa Polisi Bukombe George Kyando alithibitisha kukamatwa kwa kijana huyo na kwamba baada ya uchunguzi wa vipimo vya akili vimeonyesha ana akili timamu na taratibu zinafanyika kumfikisha mahakamani.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.