Wananchi wa kitongoji cha Bomani wamemkamata kijana mwenye miaka 28 anayedaiwa kukutwa akimnajisi bata.
Shuhuda wa tukio hilo Sacina Nangere
alisema akiwa na wenzake walisikia kelele za bata nyuma ya nyumba kwa
muda mrefu na kuamua kukimbia kuangalia kuna nini, na alipofika alimkuta
mtuhumiwa huyo akifanya kitendo hicho.
“Nilirudi kukimbia kumwita mama akaone na alipofika huyo jamaa alimtupa bata na kukimbilia kwa jirani alikokua amefikia”.
Mmiliki wa bata huyo Susana alisema
akiwa jikoni akiandaa chakula mtoto wake alimwita na kumwambia akaone
mgeni wa jirani yake anachomfanyia bata wao.
“Sikuamini
macho yangu hadi anamtupa bata na kuondoka, tulipiga yowe na wananchi
wakanisaidia kumkamata wakati akijaribu kutoroka”.
Balozi wa nyumba 1o alisema mama huyo
alifika nyumbani kwake akiwa na bata aliyenajisiwa huku akiomba msaada
na alipoangaliwa alikutwa kweli ameharibiwa na kijana huyo.
Kamanda wa Polisi Bukombe George Kyando
alithibitisha kukamatwa kwa kijana huyo na kwamba baada ya uchunguzi wa
vipimo vya akili vimeonyesha ana akili timamu na taratibu zinafanyika
kumfikisha mahakamani.


Note: Only a member of this blog may post a comment.