Mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk John Pombe Magufuli ameelezewa na
watu mbalimbali kuwa ni mchapakazi, makini, asiyependa uvivu, lakini
Rais Jakaya Kikwete amehitimisha yote kwa kumpachika jina la
“tingatinga”.
Rais Kikwete alisema hayo baada ya Magufuli kutangazwa kuwashinda makada wengine wawili waliopigiwa kura na Mkutano Mkuu wa CCM baada ya kuzoa kura 2,104, sawa na asilimia 87.08, ushindi ambao alisema unaakisi kumalizika kwa makundi yaliyoibuka kwenye mbio za kuwania kuteuliwa na CCM kugombea urais wa Serikali ya Awamu ya Tano.
Balozi Amina Salum Ali alishika nafasi ya pili kwa kupata kura 253 (sawa na asilimia 10.4), wakati Dk Asha Rose Migiro alikuwa wa mwisho kwa kupata kura 59 (asilimia 2.4). Jumla ya kura zilizopigwa kwenye mkutano huo mkuu zilikuwa 2,422 na kura sita tu ndio ziliharibika.
Rais Kikwete alisema hayo baada ya Magufuli kutangazwa kuwashinda makada wengine wawili waliopigiwa kura na Mkutano Mkuu wa CCM baada ya kuzoa kura 2,104, sawa na asilimia 87.08, ushindi ambao alisema unaakisi kumalizika kwa makundi yaliyoibuka kwenye mbio za kuwania kuteuliwa na CCM kugombea urais wa Serikali ya Awamu ya Tano.
Balozi Amina Salum Ali alishika nafasi ya pili kwa kupata kura 253 (sawa na asilimia 10.4), wakati Dk Asha Rose Migiro alikuwa wa mwisho kwa kupata kura 59 (asilimia 2.4). Jumla ya kura zilizopigwa kwenye mkutano huo mkuu zilikuwa 2,422 na kura sita tu ndio ziliharibika.
“Kila mtu anaitwa jembe,”
alisema Rais Kikwete alipokuwa akianza kutaja sifa za Magufuli ambaye
amewahi kuwa Naibu Waziri wa Ujenzi na pia Waziri wa Maendeleo ya Mifugo
na Uvuvi.
“Lakini huyu ni zaidi ya jembe. Ni tingatinga… Magufuli ni bulldozer. Magufuli havumili ujinga, ni mtu ambaye anataka kuona kazi zake zinafanyika kama alivyoagiza.”
“Lakini huyu ni zaidi ya jembe. Ni tingatinga… Magufuli ni bulldozer. Magufuli havumili ujinga, ni mtu ambaye anataka kuona kazi zake zinafanyika kama alivyoagiza.”
Kikwete aliendelea kummwagia sifa Dk Magufuli kuhusu utendaji wake
akisema kuwa alipokuwa akifuatilia wakandarasi kwenye miradi ya ujenzi,
alidiriki kuwatimua pale alipobaini walikuwa wakifanya kazi kinyume na
makubaliano.
“Tunaamini kuwa utawaongoza Watanzania vizuri,” alisema Kikwete akimgeukia mbunge huyo wa Chato.
“Tunaamini kuwa utawaongoza Watanzania vizuri,” alisema Kikwete akimgeukia mbunge huyo wa Chato.
“Tulikuwa na wagombea 338
lakini sasa tunaye mmoja na tuna kundi moja tu la CCM. Timu Magufuli
imeshaondoka. Wengi walidhani CCM itafia hapa, lakini ushindi huu ni
ishara kuwa CCM ni moja.
“Tunatakiwa kuacha kuteuwa watu kwa urafiki na kujuana ili tushinde kwa sababu imani huzaa imani. Sina shaka kuwa tutashinda lakini ushindi hauji hivi hivi lazima tuwe na mikakati mizuri, mipango thabiti na utekelezaji makini,” alisema.
Rais Kikwete ni mmoja kati ya watu wengi waliohojiwa na Mwananchi kuhusu mteule huyo wa CCM, ambaye hakuwa akitajwa kama kinara kwenye mbio za urais kabla ya kufikia hatua hiyo ya kujadiliwa na vikao vya juu.
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Mhandisi Mussa Iyombe, aliyefanya kazi na Dk Magufuli kwa zaidi ya miaka 10, alisema iwapo atachaguliwa kuwa rais basi wavivu wajitayarishe kukimbia kwani Waziri huyo ni mchapa kazi wa hali ya juu.
“Tunatakiwa kuacha kuteuwa watu kwa urafiki na kujuana ili tushinde kwa sababu imani huzaa imani. Sina shaka kuwa tutashinda lakini ushindi hauji hivi hivi lazima tuwe na mikakati mizuri, mipango thabiti na utekelezaji makini,” alisema.
Rais Kikwete ni mmoja kati ya watu wengi waliohojiwa na Mwananchi kuhusu mteule huyo wa CCM, ambaye hakuwa akitajwa kama kinara kwenye mbio za urais kabla ya kufikia hatua hiyo ya kujadiliwa na vikao vya juu.
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Mhandisi Mussa Iyombe, aliyefanya kazi na Dk Magufuli kwa zaidi ya miaka 10, alisema iwapo atachaguliwa kuwa rais basi wavivu wajitayarishe kukimbia kwani Waziri huyo ni mchapa kazi wa hali ya juu.


Note: Only a member of this blog may post a comment.