Aliyekuwa mgombea mtarajiwa wa urais nchini kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Edward Lowassa.
Na Omary Mdose, LushotoBAADA ya aliyekuwa mgombea mtarajiwa wa urais nchini kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Edward Lowassa jina lake kukatwa kwenye nafasi hiyo, hali ilibadilika kwenye mazoezi ya Simba yaliyofanyika juzi Jumamosi kwenye Uwanja wa Chuo cha Magamba, Lushoto, Tanga.
Wachezaji wa timu ya Simaba wakiwa mazoezini.
Jina la Lowassa lilikatwa usiku wa kuamkia Jumamosi ambapo awali
wachezaji na makocha wa Simba walipofika uwanjani hapo kwa ajili ya
mazoezi walikuwa hawajapata taarifa zozote kuhusiana na jambo hilo
ambapo shabiki mmoja aliibuka na kusema kwa nguvu ishu hiyo ndipo kila
mmoja wao akashtuka.Championi Jumatatu ambalo limeweka kambi maeneo haya, lilishuhudia tukio hilo ambapo baada ya kila mmoja kupata taarifa hizo akaanza kusema lake.
Wapo waliokuwa wakishangilia huku wengine wakikasirika ambapo wakati mazoezi yakiendelea jina la Lowassa lilikuwa likitajwa kila wakati hali ambayo iliwashtua wengi.
Hawakuishia hapo kwani waliendelea kutaniana huku wengine wakiitwa timu Lowassa ambapo kitendo hicho hakikukasirikiwa na kocha bali ilichukuliwa kama utani tu.
CCM imempitisha Dk John Pombe Magufuli kuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho.

Note: Only a member of this blog may post a comment.