Masistaduu wawili wa sinema za
Kibongo, Shamsa Ford na Halima Yahya ‘Davina’ wameangusha sebene la
nguvu katika Viwanja vya Ngome Kongwe walipokwenda kwa ajili ya
kuhudhuria Tamasha la Filamu la Kimataifa (ZIFF).
Katika tukio hilo lililojiri wikiendi
iliyopita, wasanii hao walikuwa wakiburudika na Wimbo wa Nani Kama Mama
wa Christian Bella uliowafanya walisakate sebene vya kutosha huku baadhi
ya watu waliokuwa pembeni yao wakiangalia burudani jukwaani kuacha na
kuwatazama wao.
Kucheza kwa wasanii hao kuliwahamasisha
wengine kuinuka kwenye viti na kuanza kucheza huku baadhi ya watu
wakiwazunguka na kuwashangilia na wengine kuwarushia fedha.

Note: Only a member of this blog may post a comment.