Rapper Young Dee amesema amewahi kujutia kuwa mtu maarufu kutokana na kukosa pesa zinazolingana na jina lake.
Akiongea na E-News ya EATV, Young Dee alisema,” Tokea nimekuwa Young
Dar es Salaam, sijawahi kujuta lakini nilijuta nilivyokuwa Young Dee
mwanzo wakati naanza. Si unajua ndo nilikuwa nimetoa ngoma yangu ya
kwanza halafu bado sina kitu alafu inabidi upande daladala halafu
unakutana na madenti wamekaa siti ya nyuma wanaanza ‘Young Dee’
wanazingua kweli yaani.”
“Ile ilikuwa inanitesa sana maana nilikuwa naona nashindwa kuwa huru
na maisha yangu yaani kuwa mtu wa kawaida tu nikapanda daladala nikakaa
poa tu. Lakini ilikuwa ngumu hiyo hali ilikuwa inanitesa sana kipindi
cha nyuma.”
-bongo5

Note: Only a member of this blog may post a comment.