Muimbaji na muandishi wa nyimbo, Barnaba baada ya kukosa tuzo ya
Mtunzi Bora wa Mwaka- Bongo Fleva kwenye KTMA 2015, ameitumia kama
changamoto na kutangaza kutoa album mwaka huu ili kuwafanya hata wale
ambao hawakumuelewa wamuelewe zaidi.
Barnaba alitumia ukurasa wake wa Instagram kuwashukuru mashabiki
waliompigia kura pamoja na wasanii wenzake aliokuwa akiwania nao
kipengele kimoja, na mwisho kuweka ahadi ya kutoa album.
Hiki ndicho alichokiandika:
“Nawashukuru watu wangu wote na mashabiki Zangu mlionipiga Kura
naamini kila kilichotokea Kimestahiri Kutokana Mimi nampenda mungu na
naamini kuna Kitu kinaitwa Wakati au muda na napenda Changamoto mana hii
Itafanya Nifanye Vyema mara mbili ya pale ninapofanyaga Yes Of coz mimi
sinaga Team Bali Team yangu ni wale wote wanaopenda Muziki Mzuri
nawapenda wote na nawapa Ongera wenzangu wote mlioshinda Bila kusahau
kipenzi Changu #bestfemaleperformer and #bestfemaleartist @Vanessamdee
Kushinda kwako ni wazi inaonesha wazi kazi nzuri Aya Tunaendelea na kazi
Ya kuangusha Vyuma Juu Ya Vyuma na mwaka Huu natoa #Album Ambayo
itafanya Yule asiyemwelewa Barnaba ajue na aelewe mwisho nawakumbusha
Umoja ni nguvu utengano…………. Tusijenge Matabaka Nndugu zangu”

Note: Only a member of this blog may post a comment.