Mahakama ya Wilaya ya Mpanda, Katavi imemuhukumu mwalimu mstaafu wa shule ya msingi Mpanda Ndogo , Rashid Ndogo mwenye miaka 65 kifungo cha maisha jela baada ya kumbala mjuu wake wa miaka mitano na kumuharibu vibaya sehemu zake za siri.
Hukumu hiyo ilitolewa jana na hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda, Chiganga Ntengwa baada ya mahakama kuridhika na ushahidi uliotolewa na pande zote mbili za mashtaka na utetezi.
Awali katika kesi hiyo mwendesha
mashtaka alidai mahakamani kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Oktoba
mwaka jana majira ya saa 2 na nusu usiku nyumbani kwake katika kijiji
cha Majalila.
Siku hiyo mshatakiwa alidaiwa kumbaka
mjuu wake wakati amelala chumbani akiwa na mtoto wa mshtakiwa ambaye
alishugudia baba yake akitenda kosa hilo la kinyama.
Siku ya tukio mke wa mshatakiwa alimwaga
mume wake kuwa amekwenda kufunga zizi la mbuzi lililokuwa jirani na
nyumbani kwao na mumewe kutumia mwanya huo kuingia chumbani kwa mjuu
wake na kuanza kumbaka huku mwanaye akishuhudia.
Mshakiwa alikamatwa na majirani siku
hiyo na kupelekwa kituo cha Polisi ambapo alifunguliwa mashtaka huku
mjukuu wake akikimbizwa hospitali kupatiwa matibabu.


Note: Only a member of this blog may post a comment.