Brighton Masalu
Sorry! Staa wa sinema za Kibongo, Halima Yahya ‘Davina’
anadaiwa kumwangukia mumewe, Abdallah Shakoor ili kurejesha uhai wa ndoa
yao ‘iliyokwaruzwa na makucha ya shetani’ ikiwa ni njia ya kurudisha
heshima na hadhi yake kwenye familia na jamii kwa jumla.
“Davina amekubali yaishe, unajua anampenda sana mumewe, ‘so’ anahaha kwa ndugu ili wamuombee msamaha,” alisema ‘kikulacho’ huyo wa Davina.
Baada ya kuudaka ‘ubuyu’ huo, Ijumaa Wikienda lilizungumza na Davina ambapo alikuwa na haya ya kusema: “Hayo ni maisha yangu binafsi, hayamhusu mtu, kwanza nipo kwenye kikao, niache.”

Note: Only a member of this blog may post a comment.