Saturday, June 20, 2015

Anonymous

MAJANGA: Mwanamke Mtanzania Akamatwa na Madawa ya Kulevya 75Kg Uwanja wa Ndege!

Mwanamke mmoja anayedaiwa kuwa Mtanzania amekamatwa na dawa za kulevya zenye uzito wa kilo 75 katika Uwanja wa Ndege India ambapo mwanamke huyo alikamatwa akiwa na hati ya kusafiria ya Tanzania. 

Mwanamke huyo alikamatwa katika Uwanja huo ambapo aligundulika kubeba mzigo huo baada ya mbwa kunusa mizigo yake akiwa eneo la upekuzi. 

Milind Lanjewar ambaye ni Ofisa wa Uwanja huo amesema hicho ni kiwango kikubwa zaidi cha dawa za kulevya kukamatwa katika kipindi cha hivi karibuni.
Lanjewar amesema mwanamke huyo alikuwa na mzigo wa unga ambao ni dawa za kulevya aina ya Methaqualone au Mandrax na Cocaine.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.