Waziri Dk. Harrison Mwakyembe amekuwa kada wa 37 kuchukua fomu ya kugombea Urais CCM katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015.
Dk. Mwakyembe amesononeshwa na mikakati miovu dhidi ya Lowassa wakati alipokuwa akijibu swali kama ana kinyongo na Lowassa.
“Naapa
mbele ya MUNGU sina chuki na mtu yoyote kwa kuwa lile suala (RICHMOND)
halikuwa langu bali lilikuwa la Bunge… Kumtaja MUNGU ni vibaya sana,
nikisema uongo atanilaani”—Dk. Mwakyembe.
Waziri Mwakyembe amesema huwa anasononeshwa na baadhi ya watu wanaosambaza maneno kuwa bado ana chuki na Lowassa na alishtushwa kupigiwa simu kwamba anatumia mitandao ya kijamii kumchafua.
“Niliripoti Polisi na TCRA na nilipata
Ushirikiano uliofanikisha baadhi ya wahusika kukamatwa.. kibaya zaidi
mmoja ya waliokamatwa ni mpambe wa Wanaogombea Urais”—Dk. Mwakyembe.


Note: Only a member of this blog may post a comment.