MTANGAZAJI na mwanamitindo, Karrueche Tran amemchana mpenzi wake wa zamani, Christopher Maurice ‘Chris Brown’ katika mitandao ya kijamii.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Karrueche alimfungukia Chris kuwa asimfuatefuate kwani mapenzi yao yalishakwisha tangu alipogundua kuwa amezaa na mwanamke mwingine.“
@chrisbrownofficial ulifanya mahojiano na Ryan Seacrest na ukaniongelea na ndiyo maana hata nilipofanyiwa mahojiano na Access Hollywood niliulizwa kuhusu wewe na nilijibu kama mtu aliyepevuka.“Niliongelea maisha yangu. Sikukuongelea. Usiwe mpumbavu wakati unajua uhusiano wetu ulikosa uaminifu.”

Note: Only a member of this blog may post a comment.