Thursday, May 28, 2015

Anonymous

VIDEO: Huwezi kuamini kama huu ni msiba, mke wa marehemu akavalishwa na shela kabisa!

Bibi harusi
Sio tukio la kawaida kukutana na mtu kavaa gauni la harusi kwenye mazishi.. kwenye headlines za 254 jirani zetu wa nguvu Kenya kuna hii stori kutoka Kaunti ya Vihiga, unaambiwa mwanamke aliyefiwa na mume wake akalazimishwa kuvaa gauni ambalo anavaa bibi harusi wakati wa kufunga ndoa, alafu safari ya kwenda kwenye mazishi ikaanza. 

Mary Akatsa ni kiongozi wa Kanisa la Jerusalem Church of Christ alikuwa akiongoza kila kitu mpaka mazishi yalipoisha, ukicheki kwenye hii video huyo mama anaonekana mkali hivi kama unaenda tofauti na maagizo yake.. wengine wanapigwa mpaka vibao.

Mazishi yalikuwa kama sherehe tu, kama ukiiona hii video unaweza kuhisi labda watu walikuwa kwenye harusi au sherehe nyingine ya kawaida. 
Unaambiwa huu ni utaratibu wa kawaida kabisa kwa waumini wote wa kanisa hilo, ikitokea mwanamke kafiwa na mume wake lazima avae shela la harusi siku ya mazishi ya mume wake.
Bonyeza play au download video hiyo hapa chini....

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.