Mtoto mchanga wa kiume wa siku tatu
katika mtaa wa Masanga Wilaya ya Igunga ameokotwa akiwa amekatwa viungo
vyake na watu wasiojulikana.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Masanga Julius Kitundu alisema mtoto huyo aliokotwa na wasamaria wema pembezoni mwa barabara ya lami.
“Kwa
kweli kitendo kama hiki kimetusikitisha na watu waliofanya kitendo hicho
wanapaswa kusakwa kwa nguvu zote na kufikishwa kwenye vyombo husika” Kitundu.
Mwenyekiti huyo alitoa wito kwa wananchi
kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi na kuwaomba watoe
ushirikiano kwa jeshi la Polisi katika kuwasaka wahusika.
Baadhi ya wananchi wamelaani kitendo
hicho cha kinyama na kusema wataanzisha msako mkali ili kuhakikisha
waliohusika wanakamatwa na mama aliyejifungua anashikiliwa.


Note: Only a member of this blog may post a comment.