Friday, May 29, 2015

Anonymous

MASTAA WA TZ NI WATU WA AJABU SANA! WALIPULIWA LIVE MISA YA MAREHEMU RECHO!

Marehemu Rachel Haule
Na Hamida Hassan
Mkurugenzi wa Kampuni ya Five Effects, William Mtitu hivi karibuni aliwalipua wasanii wenzake na kusema kuwa inavyoonekana kwa Mungu hawapo kwani wamekuwa wakichenga kwenda kanisani na msikitini inapotokea kuna kisomo kwa ajili ya marehemu.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Five Effects, William Mtitu.
Mtitu alizungumza hayo alipokuwa makaburini Kinondoni jijini Dar, kwenye misa ya mwaka mmoja ya marehemu Rachel Haule  ambapo wasanii walifika makaburini kwa wingi lakini kanisani hawakwenda.
“Yaani watu wameibuka kaburini, kwa nini hawakwenda kanisani? Mastaa ni watu wa ajabu sana, inavyoonekana hawapo kabisa kwa Mungu, hili ni jambo la kusikitisha kabisa na kwa kweli tunatakiwa kubadilika,” alisema Mtitu.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.