Saturday, May 30, 2015

Anonymous

Maneno MACHAFU Yananipa Chakula -Riyama Afunguka!

Staa wa Bongo Movies mwenye heshima kubwa kwenye tasnia ya filamu za Bongo, Riyama Ally, ameibuka na kujivunia kwamba maneno machafu anayoyatumia katika filamu mbalimbali anazocheza ndiyo yanayompa chakula cha kila siku.

Riyama alisema katika filamu mbalimbali alizocheza amekuwa akitumia maneno ya kashfa, kejeli ambayo yameonyesha kuvutia waongozaji wengi wa filamu nchini kumtumia katika filamu zao.

“Nina kila sababu ya kujivunia maneno machafu ya uswahilini kwani hayo ndiyo yananifanya nipate mialiko mingi ya kuigiza kama nilivyoshirikishwa kwenye filamu mbalimbali na sasa naheshimika kwa maneno hayo ingawa wapo baadhi wanafikiri ndiyo maisha yangu halisi wakati naigiza,” alijieleza Riyama ambaye kwa sasa anatamba katika filamu ya Uwoga.
-Mtanzania

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.