Picha hii ni ya mechi ya kwanza!
'MNYAMA' AENDELEZA 'UTEJA' KWA MBEYA CITYTimu ya Simba SC leo imeshangazwa tena na Mbeya City kwa kuchapwa mabao 2-0 katika mchezo wa ligi kuu TZ Bara uliopigwa Sokoine mkoani Mbeya.
Licha ya Simba kucheza vizuri katika kipindi cha kwanza, imekumbana na aibu hiyo kipindi cha pili kwa mabao ya Paul Nonga na Peter Malyanzi.
Kwa matokeo hayo Simba imezidi kupoteza matumaini ya mashabiki wake ya kushika nafasi ya pili kwa kuwa sasa tofauti ya point kati yake na Azam imekuwa ni point 7 kwa kuwa Azam leo imefikisha point 42 na Simba imebaki na point zake 35.
Mechi ya Simba inayofuata ni dhidi ya Azam FC itakayofanyika mwishoni mwa wiki hii.
matokeo yote ya mechi za leo ni:
Mbeya City 2-0 Simba
@Azamfc 2-1 Kagera Sugar
Stand United 1-1 JKT Ruvu
Polisi Morogoro 2-0 Ndanda
Kwa mtazamo wako, Simba itaweza kushika nafasi ya Pili?
Mbeya City 2-0 Simba
@Azamfc 2-1 Kagera Sugar
Stand United 1-1 JKT Ruvu
Polisi Morogoro 2-0 Ndanda
Kwa mtazamo wako, Simba itaweza kushika nafasi ya Pili?


Note: Only a member of this blog may post a comment.