Wednesday, April 15, 2015

Anonymous

UMEIPATA HII YA WATU KUZIKANA JUU YA MAKABURI? STORI NZIMA IPO HAPA MDAU...

Watu wanaoishi Njoro Kaunti ya Nakuru, Kenya wameiomba Serikali ya nchi hiyo kuwasaidia eneo la kufanyia mazishi kutokana na uhaba wa ardhi.

Ishu ni kwamba kutokana na maeneo ya makaburi kutotosha watu wamejikuta wakilazimika kuchimba makaburi yenye vina vifupi juu ya makaburi mengine ili waweze kufanya mazishi.

“Serikali itupatie mahali ambapo tunaweza kuzika watu wetu kwa amani.. sio ukizika ukienda kulima unapata umefufua mtu mwingine… mnarudi mnamuweka pembeni hata yeye hilo kaburi lilinunuliwa ilipaswa na yeye aweze kuzikwa”– alisema mmoja wa wakazi wa eneo hilo.
Ukosefu wa ardhi ya kuzikia ni taatizo kubwa linalokumba maeneo mengi nchini humo.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.