Baadhi ya  wananchi  wa  mjini Iringa na abiria  wa basi la Embakasy  wakitazama basi hilo  lililopinduka leo eneo la Ipogolo mjini Iringa 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
AJALI yaua mmoja Iringa huku abiria 18 wakinusurika kifo baada ya basi la kampuni ya Embakasy lenye namba za usajili T 997 AKJ kuacha njia ya kupinduka eneo la Ipogolo mjini Iringa.
 
Wakizungumza na mtandao huu eneo la ajali baadhi ya abiria wa basi hilo walidai kuwa basi hilo lilikuwa likitaka kuingia katika kituo kimoja wapo cha mafuta eneo hilo na wakati likitoka ndipo liliponusurika kugongana na lori lililokuwa barabara kuu ya Iringa - Mbeya .
 
Hivyo kutokana na kunusurika kugongana ndipo dereva wa basi hilo alipoamua kulikwepa lori hilo kwa kukata kona kubwa zaidi iliyopelekea basi hilo kuacha njia na kupinduka kando ya barabara hiyo .
 
Walisema kuwa basi hilo limekuwa likifanya safari zake kati ya Ilandutwa wilaya ya Iringa vijijini na Iringa mjini na kuwa pona yao katika ajali hiyo ni kutokana na kuwa katika mwendo wa kawaida zaidi .
 
Konda wa basi hilo Bw Esack Mtandi alielezea tukio hilo alisema kuwa basi hilo lilikuwa likitaka kuingia kujaza mafuta katika kituo kimoja wapo cha mafuta kilichopo eneo hilo na mbele kulikuwa na lori na wakati dereva akijiandaa kuingia kituoni hapo ghafla usukani uligoma na hivyo kumtoa dereva nje ya barabara kabla ya kupinduka.
AJALI yaua mmoja Iringa huku abiria 18 wakinusurika kifo baada ya basi la kampuni ya Embakasy lenye namba za usajili T 997 AKJ kuacha njia ya kupinduka eneo la Ipogolo mjini Iringa.
Wakizungumza na mtandao huu eneo la ajali baadhi ya abiria wa basi hilo walidai kuwa basi hilo lilikuwa likitaka kuingia katika kituo kimoja wapo cha mafuta eneo hilo na wakati likitoka ndipo liliponusurika kugongana na lori lililokuwa barabara kuu ya Iringa - Mbeya .
Hivyo kutokana na kunusurika kugongana ndipo dereva wa basi hilo alipoamua kulikwepa lori hilo kwa kukata kona kubwa zaidi iliyopelekea basi hilo kuacha njia na kupinduka kando ya barabara hiyo .
Walisema kuwa basi hilo limekuwa likifanya safari zake kati ya Ilandutwa wilaya ya Iringa vijijini na Iringa mjini na kuwa pona yao katika ajali hiyo ni kutokana na kuwa katika mwendo wa kawaida zaidi .
Konda wa basi hilo Bw Esack Mtandi alielezea tukio hilo alisema kuwa basi hilo lilikuwa likitaka kuingia kujaza mafuta katika kituo kimoja wapo cha mafuta kilichopo eneo hilo na mbele kulikuwa na lori na wakati dereva akijiandaa kuingia kituoni hapo ghafla usukani uligoma na hivyo kumtoa dereva nje ya barabara kabla ya kupinduka.
Alisema  katika basi  hilo kati ya abiria  18  waliokuwepo  abiria  6  ndio  waliojeruhiwa akiwemo  dereva na  hakuna  aliyepoteza maisha.
Kwa  upande  wake  jeshi la  polisi  mkoani Iringa  limethibitisha  kutokea kwa ajali hiyo na  kuwa  ajali   hiyo  ilitokea majira  ya saa 3  kasoro asubuhi ya  leo   na  kumtaja  dereva  wa  basi hilo  kuwa ni Abdalah Nyalusi.
Alisema  kamanda  wa  polisi  mkoa  wa  Iringa Ramadhan  Mungi na  kuwa katika  ajali  hiyo  hakuna abiria  aliyepoteza maisha . 
   
Wakati huo huo mmoja kati ya wafanyabiashara maarufu mji wa Ilula wilayani Kilolo mkoani hapa aliyefahakika kwa jina moja la kasim aliyekuwa akiendesha gari lenye namba za usajili T 111 GRE RAV4 amekufa papo hapo baada ya kugongana uso kwa uso la lori.
Wakati huo huo mmoja kati ya wafanyabiashara maarufu mji wa Ilula wilayani Kilolo mkoani hapa aliyefahakika kwa jina moja la kasim aliyekuwa akiendesha gari lenye namba za usajili T 111 GRE RAV4 amekufa papo hapo baada ya kugongana uso kwa uso la lori.
Kamanda  Mungi  alisema  kuwa mfanyabiashara   huyo  alikuwa  akitokea  Ilula  kuja  Iringa  mjini na baada ta  kufika  eneo la kona  ya Igumbilo  barabara  kuu ya  Iringa - Dar es salaam  wakati  akijaribu kulipita daladala  lililokuwa mbele yake  katika  kona    hiyo ghafla  alikutana na lori  hilo na kugongana  nalo . 
 
Hata hivyo alisema jina kamili la mtu huyo bado kufahamika na kuwa wanasubiri ndugu zake ili kujakutambua mwili huo na kutoa jina kamili.
Hata hivyo alisema jina kamili la mtu huyo bado kufahamika na kuwa wanasubiri ndugu zake ili kujakutambua mwili huo na kutoa jina kamili.

Note: Only a member of this blog may post a comment.