Jeshi la Polisi Kanda Maalum DAR limesema wafuasi wa Askofu Gwajima
ni marufuku kutia mguu eneo atakalohojiwa Askofu huyo, ambapo kauli
hiyo imekuja siku chache baada ya Askofu huyo kuwataka wafuasi hao
kumsindikiza kuelekea kituoni hapo.
“Napenda
kutumia nafasi hii kumuomba GWAJIMA awaambie wafuasi wake hawahitajiki
kufika eneo hilo.. anayehitajika ni yeye na Mwanasheria wake”—Kamanda Suleiman Kova.
Kamanda Kova amesema iwapo kila mtu atafuata taratibu hakuna nguvu itakayotumika.


Note: Only a member of this blog may post a comment.