Akizungumzia Hekaheka ambayo iliwahi kukutana nayo kuna siku walienda Shinyanga kwenye michezo ya jadi kitaifa akakutana na dada mmoja ambae alitaka kufanya filamu, katika kutumiana ujumbe mume wake akaona akampigia simu na kumtuhumu kutembea na mke wake akamweleza walikuwa wanawasiliana kuhusu filamu waliyotaka watengeneze, jamaa huyo hakumuelewa na kumtishia kumuua ingawa hakuogopa lakini badae alizungumza na mke wake akamwambia yameisha.
Kuhusu watu ambao anapenda kucheza nao kwenye filamu amesema anaelewana sana na Bi staa kutokana na kuanza wote sanaa, kuhusu kazi alizofanya amesema anapenda sana Tamthilia ya Fukuto na kwa upande wa filamu anapenda sana filamu ya Kigodoro.
Bonyeza play kusikilia Hekaheka yote mtu wangu… -via millardayo


Note: Only a member of this blog may post a comment.