Tuesday, March 24, 2015

Anonymous

Kidoti na brand maalum, Collabo ya Vee Money na Muigizaji Wema Sepetu na biashara za mitandaoni#255CloudsFM

Baada ya watu  kuhoji  ishu ya kampuni ya Kidoti kutengeneza ndala ambazo ni maalum kwa wanawake na kuonekama kama amewasahau wanaume, 255 imemtafuta Jokate ambae amesema kutakuwa na brand maalum ya wanaume na wataanza kuzipata muda wowote, akizungumzia kuhusu bei kuwa juu amesema watu wanaochukua ndio wanapandisha bei kutokana na gharama za kwenda kuzichukua.
Screenshot-2014-06-20-at-00.00.45
Mwanamziki  Vee Money wiki hii anategemea kuachia ngoma mpya aliyomshirikisha Rapa kutoka Afrika Kusini KO, akizungumzia ngoma hiyo amesema ni wimbo unaohusu mapenzi ya dhati ambao ni maalum kwa watu wote wanaopendana, kuhusu kumshirikisha KO amesema alikuwa anatamani kufanyanae kazi kwa muda mrefu lakini hakuwa na uhakika kama atapata ushirikiano lakini aliweza kuzungumza nae na kufanikiwa kufanya nae kazi.
wema_sepetu
Muigizaji Wema Sepetu amesema mitandao ya kijamii inanafasi kubwa katika maisha yake hasa katika maswala ya utangazaji na kutolea mfano mtandao wa Instagram na kusema, umerahisisha kazi kutokana na kutumiwa sana katika matangazo, yeye ameweza kujua maduka mengi na vitu vingi kupitia mtandao huo na endapo mtu akitaka apost kazi yake kwenye page yake ni kama dola elfu moja au elfu mbili lakini inategemea na makubaliano.
-via millardayo

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.