Monday, March 2, 2015

Anonymous

DUH! KUMBE MTOTO MZURI SHAMSA FORD ALIKUTANA NA MUMEWE KIAJABU

Na Andrew Carlos/ijumaawikienda
STAA wa filamu Bongo, Shamsa Ford amefungukia uhusiano wake kwa mara ya kwanza na mumewe, Dickson Matoke kwamba walikutana kiajabuajabu na kuwa wapenzi.
Staa wa filamu Bongo, Shamsa Ford
Akizungumza katika mahojiano maalum na Kipindi cha Me and You With Love kilichofanywa na Global TV hivi karibuni, Shamsa alisema kuwa siku ya kwanza hakudhani kama Dick ndiye atakuwa mumewe kwani walikuwa wakikutana katika kumbi za starehe tu. 

“Siku ya kwanza tulibadilishana namba na ukawa ndiyo kama mchezo, kila tukitaka kwenda kwenye starehe alikuwa akinipigia simu hadi ikawa mazoea na kujikuta tukiangukia katika penzi,” alisema Shamsa.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.