Thursday, February 12, 2015

Anonymous

MAAJABU! Hawa watoto wamepishana miezi miwili kuzaliwa, eti nao wanaitwa mapacha?!

Watoto hawa wanaweza kuitwa mapacha wa miujiza baada ya kuwashangaza madaktari kutokana na kupishana kwao muda wa kuzaliwa. 

Watoto hao walizaliwa katika moja ya hospitali huko Romania, sio kwamba wametofautiana miezi miwili kuzaliwa pia wametofautiana miaka kwani mmoja alizaliwa November 2014, mama huyo alilazimika kukaa chumba cha kujifungulia hadi Januari 2015 ndipo akazaliwa mtoto mwingine. 

Madaktari walishangazwa na hali hiyo kwa kuwa si ya kawaida, walitegemea watoto hao wangezaliwa siku moja kama ilivyo kawaida lakini haikuwa hivyo. 

Kwa mujibu wa wataalamu walisema watoto hao walizaliwa katika mifuko tofauti ya uzazi ambayo iliruhusu mmoja kuzaliwa kabla ya mwenzake.
JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142.ASANTE NA KARIBU TENA! 

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.