Friday, February 6, 2015

Anonymous

MAADUI WEMA SEPETU NA DADA 'AKE DIAMOND PLATINUMZ SASA MAMBO MMWAAA..!

Wema Sepetu na mdogo wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’ ambaye ni mke wa Petit Man, Esma Khan.
Na Imelda Mtema
Msanii wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel amefanya kazi ya ziada kuhakikisha shoga yake, Wema Sepetu na mdogo wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’ ambaye ni mke wa Petit Man, Esma Khan wanapatana. 

Chanzo chetu kilichokaribu na mastaa hao kilieleza kuwa, awali Wema na Esma walikuwa hawaivi lakini juzi Aunt aliwakalisha na kuwataka wamalize tofauti zao ambapo kila mmoja aliona ni heri iwe hivyo.
 “Si unajua Wema na yule wifi yake Esma walikuwa hawaivi tangu Diamond aamue kuachana naye?

Wema Sepetu akiwa na shoga yake Aunt Ezekiel.
Kimsingi walifikia hatua mbaya, huwezi kuamini kama ni wale waliokuwa wanaitana wifi lakini juzi Aunt kafanikiwa kuwapatanisha,” kilidai chanzo hicho kilichoomba hifadhi ya jina lake.

Baada ya kuzipata habari hizo, mwandishi wetu aliwatafuta Wema na Esma bila mafanikio lakini Aunt alipatikana na kukiri kufanya kazi hiyo.
JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142.ASANTE NA KARIBU TENA! 

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.