Wednesday, February 25, 2015

Anonymous

KWISHNEI! NDOA YA SLIM YAVUNJWA MAHAKAMANI

IMELDA MTEMA/Mchanganyiko
NDOA ya staa wa filamu nchini, Salim Mbegu ‘Slim’ na mkewe Asia Morgan imevunjwa rasmi na Mahakama ya Mwanzo ya Magomeni jijini Dar kufuatia mgogoro wa muda mrefu. 

“Mahakama hii imevunja baada ya mdai (mke) kusema hata iweje hawezi kurudi tena kwa mumewe huyo kutokana na kuwa na wivu wa kupindukia na kingine kibaya walivyokuwa kwenye mgogoro kuna mwanamke alikuwa akijinadi  kwa kupiga picha nyumbani kwa mumewe na kuzituma kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram,” alisema Hakimu Mwanaidi Madeni wa mahakama hiyo. 

Hakimu aliamuru watalaka hao kugawana mali zote walizochuma pamoja likiwemo gari walilozawadiwa wakati wa harusi yao, ambalo ndilo lilikuwa chanzo cha mgogoro huo.Wakati mume akisema anaiheshimu hukumu hiyo ingawa anaona kama ni filamu, mke alionyesha furaha yake na kudai sasa ataishi kwa amani.
JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142. 
ASANTE NA KARIBU TENA!

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.