Mbio za kuusaka urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),
zimezidi kupamba moto baada ya kundi la wabunge wapatao 150 kujitokeza
hadharani na kueleza kumuunga mkono mmoja wa wanaotajwa kuwa wagombea, Edward Lowassa, wakimtaka kujitosa kwenye kinyang’anyiro hicho.
Hali hiyo inajitokeza wakati wa Mkutano
wa Bunge wa 18 ukihitimishwa mwishoni mwa wiki na kubakia miwili tu
Bunge la 10 kufikia tamati, hivyo kwa kila hali uchaguzi mkuu kuzidi
kunukia kazi kubwa ikiwa ni kupatikana kwa rais wa tano wa Tanzania.
Kwa kitambo sasa kumekuwa na makundi
yanayosigana kila moja likiwa na mgombea wake, hata hivyo mpambano
mkubwa wa kumpata mgombea unaonekana kuwa zaidi ndani ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM), kurithi mikoba ya Rais Jakaya Kikwete, anayehitimisha uongozi wake wa utawala Oktoba mwaka huu kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katika mbio hizo, sasa ni rasmi kwamba
kundi la wabunge wanaodaiwa kufikia 150 walikutana katika chakula cha
jioni mjini Dodoma eneo la Kilimani mwishoni wiki iliyopita wote
waliopata fursa ya kuzungumza katika hafla hiyo, walisema wazi kuwa
wanamuunga mkono Lowassa katika mbio za urais.
Lowassa ambaye pia ni mbunge wa Monduli
na Waziri Mkuu wa zamani, anadaiwa kutakiwa na wabunge hao kuwa muda
ukifika achukue fomu za kuwania urais kwa tiketi ya CCM katika uchaguzi
mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.
Ingawa kumekuwa na tetesi na minong’ono
ya Lowassa kuungwa mkono ndani ya CCM kuwania nafasi hiyo ya juu kabisa
ambayo pia itampa fursa ya kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, uamuzi wa
wiki iliyopita wa wabunge hao kusimama hadharani unaibua moto mkubwa wa
kinyang’anyoro cha urais huku jina la Lowassa likizidi kutajwa kama
chaguo la wengi.
JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142.ASANTE NA KARIBU TENA!
JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142.ASANTE NA KARIBU TENA!
-NIPASHE


Note: Only a member of this blog may post a comment.