Monday, February 9, 2015

Anonymous

KUMEKUCHA: WABUNGE WAMBEBA LOWASSA URAIS 2015

Mbio za kuusaka urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), zimezidi kupamba moto baada ya kundi la wabunge wapatao 150 kujitokeza hadharani na kueleza kumuunga mkono mmoja wa wanaotajwa kuwa wagombea, Edward Lowassa, wakimtaka kujitosa kwenye kinyang’anyiro hicho. 

Hali hiyo inajitokeza wakati wa Mkutano wa Bunge wa 18 ukihitimishwa mwishoni mwa wiki na kubakia miwili tu Bunge la 10 kufikia tamati, hivyo kwa kila hali uchaguzi mkuu kuzidi kunukia kazi kubwa ikiwa ni kupatikana kwa rais wa tano wa Tanzania. 
Kwa kitambo sasa kumekuwa na makundi yanayosigana kila moja likiwa na mgombea wake, hata hivyo mpambano mkubwa wa kumpata mgombea unaonekana kuwa zaidi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kurithi mikoba ya Rais Jakaya Kikwete, anayehitimisha uongozi wake wa utawala Oktoba mwaka huu kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Katika mbio hizo, sasa ni rasmi kwamba kundi la wabunge wanaodaiwa kufikia 150 walikutana katika chakula cha jioni mjini Dodoma eneo la Kilimani mwishoni wiki iliyopita wote waliopata fursa ya kuzungumza katika hafla hiyo, walisema wazi kuwa wanamuunga mkono Lowassa katika mbio za urais. 

Lowassa ambaye pia ni mbunge wa Monduli na Waziri Mkuu wa zamani, anadaiwa kutakiwa na wabunge hao kuwa muda ukifika achukue fomu za kuwania urais kwa tiketi ya CCM katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu. 

Ingawa kumekuwa na tetesi na minong’ono ya Lowassa kuungwa mkono ndani ya CCM kuwania nafasi hiyo ya juu kabisa ambayo pia itampa fursa ya kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, uamuzi wa wiki iliyopita wa wabunge hao kusimama hadharani unaibua moto mkubwa wa kinyang’anyoro cha urais huku jina la Lowassa likizidi kutajwa kama chaguo la wengi.

JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142.ASANTE NA KARIBU TENA!
-NIPASHE

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.