Nakusogezea kutoka China, wanandoa wameacha hela kwenye meza kiasi cha Yuan 300 (sawa na sh. elfu 85 Tshs) pamoja na ujumbe ambao unamtaarifu mwizi yoyote atakayeingia achukue hela hizo.
Imekuwa kawaida yao kufanya hivyo, safari hii walikuwa wakisafiri kwenda Shenzhen, Kusini mwa China safari ambayo walipanga kukaa kwa miezi miwili.
Ujumbe wa wanandoa hao pamoja na cash waliyoiacha kwenye meza yao.
Mwaka 2010 waliwahi kusafiri na kuacha pesa na ujumbe kama huo, waliporudi walikuta mlango umevunjwa na pesa zimeibiwa lakini hakuna kitu chochote kingine ambacho kimeibiwa ndani ya nyumba yao.
JIUNGE
NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU
UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142.ASANTE NA KARIBU
TENA!
-millardayo


Note: Only a member of this blog may post a comment.