Wednesday, February 11, 2015

Anonymous

JE, BOBBI KRISTINA KUTOLEWA MASHINE YA KUPUMILIA LEO?! Hii ni taarifa rasmi iliyotolewa na familia yake!


Bado kuna utata kuhusu kinaachoendelea juu ya afya ya Bobbi Kristina, mtoto wa pekee wa Marehemu Whitney Houston, mengi yanaendelea kuzungumzwa kuhusu hali yake huku wengine wakisema kuwa leo ni siku ambayo familia hiyo imeruhusu madaktari kumtoa mashine ya kupumulia ambayo aliwekewa toka siku ambayo alifikishwa hospitali baada ya kukutwa akiwa ameanguka ndani ya bafu, Georgia Marekani.
 

Baada ya yote kusikika familia ya Bobbi huyo imeamua kutumia kampuni ya wanasheria wao kutoa maelezo rasmi kuhusu kila ambacho kimesikika kuhusu hali ya mtoto huyo, taarifa hiyo imekanusha uvumi wote uliowahi kusikika ikiwemo ishu ya kumtoa mipira ya kupumulia siku ya leo ambapo ni siku ambayo mama yake alifariki. 

Katika taarifa hiyo ya Wanasheria wa familia hiyo wamesema wanaangalia namna ya kuwachukulia hatu wote waliotoa taarifa za uongo ikiwemo waliosema walizungumza na wahusika wa familia hiyo kitu ambacho sio kweli.
whitney-bobbi-kristina
Marehemu Whitney Houston akiwa na mtoto wake Bobbi Kristine wakati akiwa mdogo. 
TMZ, The National Enquirer, The Atlanta Journal Constitution na the Daily Mail ni sehemu ya vyombo vya habari ambavyo vimelaumiwa kwa kuandika taarifa za uongo.
ap_bobbi_kristina_oprah_jt_120311_wg
Bobbi Kristina akiwa na Oprah Winfrey
Bado hakuna taarifa rasmi ambayo familia hiyo imetoa kuhusu hali ya mtoto huyo, leo inatimia miaka miaka mitatu tangu afariki Whitney Houston ambaye alikutwa pia.
PICHAZ: RAIS JK AFUNGUA JENGO LA NSSF LA KITEGA UCHUMI MOSHI!
===>>JIONEE HAPA!
JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142.ASANTE NA KARIBU TENA!

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.