Monday, February 16, 2015

Anonymous

HATARI SANA! WEMA SEPETU AMRUDISHA UJANA BI. MWENDA!

Stori: Na Mwandishi Wetu/Ijumaa Wikienda 
STAA wa filamu za Kibongo, Wema Sepetu amemfanyia ‘sapraizi’ msanii mkongwe, Fatuma Makongoro ‘Bi. Mwenda’ kwa kumnunulia simu ya kisasa na kumfanya awe kama kijana.
Staa wa filamu za Kibongo, Wema Sepetu.
Wema alimfanyia sapraizi hiyo hivi karibuni kwa kummpeleka Bi.Mwenda katika maduka ya Mlimani City pasipo kumwambia wanakwenda kufanya nini na alipofika, akamnunulia simu hiyo yenye uwezo wa ‘internet’.

Msanii mkongwe, Fatuma Makongoro ‘Bi. Mwenda’.
“Namshukuru sana Wema maana sikujua tunakwenda kufanya nini Mlimani City, nikashangaa ananikabidhi simu, nimefurahi na mimi kuwa kama vijana wa kisasa, kuingia WhatsApp na Instagram,” alisema Bi. Mwenda.
JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142. 
ASANTE NA KARIBU TENA!

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.