Friday, February 13, 2015

Anonymous

#EPL WAFAHAMU MASTAA UINGEREZA WANAONGOZA KWA KUCHEZEWA RAFU!

Ligi kuu ya England inafahamika kwa jinsi ilivyo mahiri kwa matumizi ya nguvu na kasi hali ambayo hulazimu wachezaji wanaocheza ligi hii kuhakikisha wanazoea mazingira yake na mara nyingi wengi hushindwa kumudu mikimiki yake na kurudi walikotoka . 

Moja kati ya watu ambao wanaweza wakaelezea dhana hii kwa ufasaha kuliko wote ni nyota wa Chelsea Eden Hazard ambaye ametajwa kuwa mchezaji ambaye amechezewa rafu kuliko wachezaji wote kwenye ligi hii . 

Katika hali ya kawaida mtindo wa uchezaji wa Hazard unalazimu mabeki na viungo wakabaji wa timu pinzani kumchezea rafu kwani ni mchezaji mwenye kupenda sana kumiliki mpira huku akiwahadaa mabeki na wachezaji wengine wa timu pinzani kwa chenga zake za maudhi .
Eden Hazard amechewa rafu na wachezaji wa timu pinzani mara 74 , kiwango ambacho ni kikubwa kuliko vyote ka wachezaji waliochezea rafu toka timu mbalimbali katika mechi za ligi ya England . 

Katika orodha hii nafasi ya pili imekwenda kwa Raheem Sterling ambaye amechezewa rafu mara 60 na ukitazama uchezaji wa Raheem Sterling ambaye kasi yake na ujanja wa kumiliki mpira na kuwapita mabeki unawaachia wapinzani wazo moja tu la kumzuia nalo ni kumchezea rafu unaweza ukaelewa kwanini anaingia kwenye orodha hii . 

Mshambuliaji wa Everton Steven Naismith na Kiungo mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez wameingia kwenye orodha hii wakiwa kwenye nafasi ya 3 na ya 4 ambapo wamechewa rafu mara 52 na mara 47 katika mpangilio . 

WACHEZAJI WALIOCHEZEWA RAFU NYINGI EPL (2014/15)
Mchezaji                Idadi ya Rafu.
Hazard, Eden               74
Sterling, Raheem         60
Naismith, Steven         52
Sánchez, Alexis           47
Agbonlahor, Gabriel   46
Cabella, Rémy            45
Fer, Leroy                   45
Sessegnon, Stéphane   44
Colback, Jack              44
Wickham, Connor       41
Cazorla, Santiago        41
Mané, Sadio                41
Song, Alexandre         40
JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142. 
ASANTE NA KARIBU TENA!

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.