Story ya kwanza kusikika kwenye 255 leo February ilikuwa inahusu kuvuja kwa wimbo wa Diamond na Iyanya ambapo baada ya kuvuja wimbo huo watu walihisi ni collabo ya Diamond na P Square.
Kulikuwa na mvutano kwenye social networks kuhusiana na kilichoandikwa na mtangazaji mmoja TZ ambapo aliweka picha ya Chege na wasanii wenzake kwenye ukurasa wake Instagram wakiwa wamevaa tshirt zilizoandikwa RIP Mez B pamoja na vitambaa vyeusi mkononi huku kukiwa na post iliyouliza kitambaa kile cheusi kama ni hirizi.
Chege ameongea kwenye 255na kuonyeshwa kukasirishwa na kitendo hicho, alipotafutwa mtangazaji huyo amemuomba radhi Chege na kusema yeye alijua kabla hajaweka post hiyo kuwa ile sio hirizi ilikuwa ni kitambaa.
Ya mwisho kusikika ni kutoka Dodoma ambapo ndugu wa marehemu Mez B walitoa ratiba ya leo ambapo mazishi yatakuwa yakifanyika Dodoma.
JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU
UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142.
ASANTE NA KARIBU
TENA!
-millardayo


Note: Only a member of this blog may post a comment.