Thursday, December 22, 2016

Unknown

Tumbua Tumbua Sasa Yageukia Upande Huu...

Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk. Charles Tizeba amesimamisha shughuli zote za Mfuko wa Wakfu wa Kuendeleza zao la Korosho (CIDTF), baada ya kubaini mfuko huo kutumia vibaya fedha za umma na kusababisha hasara.

Pamoja na kuzuia shughuli za mfuko huo, Waziri huyo pia ameagiza viongozi wa mfuko, kutojihusisha na miamala yoyote ya mfuko huo kuanzia jana hadi pale hatma dhidi yao itakapobainishwa hapo baadaye.

Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam amesema mfuko huo umekuwa ukilalamikiwa kwa muda mrefu na wakulima na kwamba mfuko huo umebainika kutumia fedha vibaya, ikiwa ni pamoja na kutofuata maagizo ya Rais John Magufuli ya kufungua akaunti Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Sasa hivi nina taarifa kuwa mfuko huu katika benki moja wanazo fedha karibia sh. bilioni tano ambazo pamoja na kuiva, walielekezwa wazitoe huko na kuzipeleka BoT, lakini wameendelea kugoma, najiuliza kwa nini wamegoma,” alihoji waziri huyo.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.