Friday, September 16, 2016

Unknown

Jose Mourinho kutumia kikosi chake cha kawaida Man Utd dhidi ya Watford

Kocha wa Manchester United Jose Mourinho amefunguka kwamba atarejelea kikosi chake cha kawaida wakati wa mechi dhidi ya Watford baada ya kushindwa na Feyenoord mechi ya Europa League Alhamisi.
Mourinho alifanya mabadiliko ya wachezaji nane kwenye kikosi kilichocheza mechi ya Alhamisi ambapo walicheza vibaya na kufungwa 1-0. Bao lilifungwa na Tonny Vilhena dakika ya 79.

Nahodha Wayne Rooney na wachezaji wengeine Antonio Valencia na Luke Shaw walipumzishwa kwa ajili ya mechi hiyo ya Ligi ya Premia itakayochezwa Jumapili.
Mourinho amesema: “Tunarejelea kikosi cha kawaida bila mabadiliko makubwa.”

Paul Pogba alikuwepo safu ya kati lakini hakuweza kutamba.
“Huwa sitaki kuangalia wachezaji binafsi sana,” amesema Mourinho . “Ni jambo nisilopenda.”
“Nafikiri ni kama alicheza kama timu yote. Kipindi cha kwanza walidhiti mechi lakini kasi yao ilikuwa nusu. Kipindi cha pili waliongeza kasi na hapo ndipo tulifungwa.”

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.