Friday, May 20, 2016

Anonymous

Serikali na Wabunge 250 Kuogopa Hotuba ya Kurasa 30 Hawawezi Kuongoza Nchi -MSIGWA

Msigwa anasema,
''Serikali imepewa mamlaka ya kuongoza nchi na inajinadi bungeni kuwa wanaongoza vizuri na wapinzani nao wanakuja kuwarekebisha kuwa hoja zao haziwezekani , sasa serikali inayosema 'hapa kazi' inayoungwa mkono na wabunge 250 wa chama cha mapinduzi inashindwa kujibu hotuba ya kurasa 34, inataka kuwaambia nini watanzania?

Je, mpo matured kuiongoza serikali? Njooni na hoja muonyeshe udhaifu wa upinzani uko wapi, muwashawishi watanzania kuwa kweli mnaweza kuongoza lakini hamuwezi kukabiliana na hoja mnaweka mpira kwapani mnataka msaidiwe na refa ,are you fit to lead this country?

Nani asiyejua mizengwe ya nyumba zilizouzwa nchi hii? nani asiyejua nchii hii ina mikataba mibovu?''
''Huyu Rais mwema ambaye anatakiwa kushangiliwa kama King Kanuti, hatakiwi kuguswa katika bunge hili?''
Msigwa anaendelea kuongea wabunge wengine wanazomea wengine wanashangilia chaos tupu.
Sikiliza hapa:

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.