Mwanamitindo Mtanzania Millen Magese
ambaye amekua akiishi na kufanya kazi Marekani amechukua likizo ya
mwezi mmoja kufanya kampeni ya tatizo la kiafya ambalo limekua
likimsumbua toka akiwa na umri wa miaka 13 na ikaja kugundulika akiwa na
miaka 26 na mpaka sasa ameshafanyiwa Oparesheni 13 kutokana na tatizo
la Endometriosis linalomkabili kwa maumivu kila anapokuwa kwenye mzunguko wake kama Mwanamke.
Moja ya matokeo ya tatizo hili Millen
anasema ni kusababisha kutopata mtoto na baada ya kuhangaika sana na
kulipia gharama kubwa kwenye hospitali za Marekani na Afrika kusini,
sasa amepanga kuoondoa kizazi mwezi April 2016 na hatua hiyo itasaidia
afya yake kuwa na afadhali zaidi kuliko kipindi kilichopita.
Anasema ‘sitakuwa
naumwa kila mwezi, sitakuwa na mzunguko… Mungu akibariki nitaondoa
kizazi April, hii sio mara ya kwanza kutaka kuondoa kizazi ni mara ya
tatu, mara ya pili September 2015 nilifika kabisa mpaka natakiwa kuingia
kusaini ili kitolewe lakini nikasema No siko tayari, huwezi kujua Mungu
ana makusudi gani… atakaponiongoza nitakwenda ila siumii tena sababu
kuna uwezo wa Mwanamke mwingine kunibebea mtoto wangu na nikaokoa maisha
yangu kwa sababu nina mayai‘
Kuhusu kwenda kuombewa kwa muhubiri maarufu wa Nigeria TB Joshua, Millen amesema ‘Sijakwenda
kwa TB Joshua lakini ninachoamini hakuna mtu stong kuliko Mungu, imani
yangu inaweza isiwe kwenye hayo Makanisa wanayoyatamka na mimi sio mtu
wa kufata mkumbo, mimi ni Mkatoliki na nakwenda ninapotaka kwenda‘
Kumtazama Millen zaidi na kuelewa anayoyapitia unaweza kubonyeza play kwenye hii video hapa chini…
-via millardayo
Note: Only a member of this blog may post a comment.