Wednesday, March 9, 2016

Anonymous

WAZIRI UMMY ‘AMJIA JUU’ MKURUGENZI BENKI YA WANAWAKE


WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ametoa siku tatu kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB), awasilishe maelezo kwa nini benki hiyo inatoza kiwango kikubwa cha riba kwa wanawake katika mikopo, wakati inapewa fedha na Serikali kwa ajili ya kusaidia kundi hilo.

Pia waziri huyo ametangaza kiama kwa wakurugenzi wote wa halmashauri za wilaya wasiotenga asilimia tano ya bajeti yao kwa ajili ya mfuko wa maendeleo ya wanawake, kuwa kuanzia sasa, watakaoshindwa kutimiza agizo hilo, watatumbuliwa majipu. Alisema hayo jana kwenye kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, jijini Dar es Salaam.
Alisema alishitushwa na taarifa aliyopatiwa juzi katika sherehe za kukabidhi mikopo kwa wanawake zilizofanywa na Benki ya Posta Tanzania (TPB), baada ya kubaini kuwa benki hiyo ya wanawake inatoza kiasi kikubwa cha riba katika mikopo yake.

“Nilisikitika sana kusikia eti TPB inatoza vikundi vya akina mama riba ya asilimia 11 wakati benki ya wanawake inatoza riba ya zaidi ya asilimia 19. Hili siwezi kulikubali hivi inaingia akilini kweli wanawake kushangilia benki nyingine wakati ipo benki ya wanawake kwa ajili yao, tena iliyoanzishwa kwa ruzuku ya Serikali? Alihoji. 

Alimtaka Mkurugenzi wa benki hiyo, Margareth Chacha (aliyekuwepo kwenye maadhimisho hayo), kumpatia maelezo ndani ya siku tatu kwa nini benki hiyo inatoza kiwango hicho kikubwa cha riba. “Nataka mnieleze kwa nini benki hii si rafiki kwa wanawake wakati inapewa fedha na Serikali.”

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.