KIUNGO wa Yanga, Haruna Niyonzima amekuwa gumzo mjini hapa kutokana na kukubalika na mashabiki wengi wa soka jijini hapa.
Mashabiki hao walionekana kumfurahia Niyonzima kuliko nyota wengine wa kikosi hicho.
Yanga leo inacheza na APR mchezo wa raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwenye Uwanja wa Amahoro.
Championi Jumamosi lilishuhudia mashabiki kibao wakilitaja jina la kiungo huyo na kudai kuwa Yanga nzima Niyonzima ndiye wanayempenda kwa kuwa pia ni Mnyarwanda mwenzao.
Mashabiki hao walionekana kumfurahia Niyonzima kuliko nyota wengine wa kikosi hicho.
Yanga leo inacheza na APR mchezo wa raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwenye Uwanja wa Amahoro.
Championi Jumamosi lilishuhudia mashabiki kibao wakilitaja jina la kiungo huyo na kudai kuwa Yanga nzima Niyonzima ndiye wanayempenda kwa kuwa pia ni Mnyarwanda mwenzao.
Wakatio huohuo, shabiki mmoja wa Yanga ambaye ni Mtanzania jana alipata bahati ya kupiga ‘selfie’ za kutosha na mashabiki wa nchini hapa wakidhani ni kiungo wa timu hiyo, Thabani Kamusoko.
Shabiki huyo wa Yanga ambaye pia ana rasta kama Kamusoko, alipata shavu
kufuatia kuzungukwa na mashabiki wenzake ambao ni raia wa Rwanda
waliokuwa wakimpongeza kwa kazi nzuri anayoifanya katika kikosi hicho.
Licha ya shabiki huyo wa Yanga kutambua yeye siyo Kamusoko wala hakutaka kuweka wazi hilo zaidi alizidi kuonyesha manjonjo mbele ya Wanyarwanda hao ambao walionekana kuwa na mzuka wa ukweli wakidhani ni Kamusoko wa ukweli.
Licha ya shabiki huyo wa Yanga kutambua yeye siyo Kamusoko wala hakutaka kuweka wazi hilo zaidi alizidi kuonyesha manjonjo mbele ya Wanyarwanda hao ambao walionekana kuwa na mzuka wa ukweli wakidhani ni Kamusoko wa ukweli.
Note: Only a member of this blog may post a comment.