Thursday, March 10, 2016

Anonymous

Idadi Kamili ya Watanzania Waliofungwa Gereza Moja na JACKIE Cliff Nchini China



December 2013 ndio zilitoka taarifa rasmi za kukamatwa kwa Mrembo wa Kitanzania Jackie Cliff akiwa na dawa za kulevya kwenye mji wa Macao huko China ambapo alihukumiwa kutumikia miaka kadhaa gerezani.

Jackie alipata umaarufu Tanzania kupitia kuonekana kwenye video kadhaa za bongofleva kama ‘she got a gwan‘ ya Marehemu Ngwea na hata nyingine ya Linex ‘kamugina‘ na baada ya kuripotiwa kukamatwa, kila mmoja akataka kujua kilichotokea na kinachofatia.

Jackie Cliff

Kama sio Jackie Cliff basi inawezekana leo tusingekua tunafahamu ni Watanzania wangapi waliofungwa kwenye gereza moja na yeye kwenye mjia wa Macao… idadi niliyopewa ni 12 ambapo Mtanzania Wabogojo anayeishi na kufanya kazi kwenye mji huohuo wa Macao amesema Wanawake ni wawili tu, Jackie na mwenzie aliyekamatwa karibuni…. huwa anakwenda kuwatembelea Watanzania wote kila Jumamosi.

Wabogojo amesema ‘kila Jumamosi huwa nakwenda kuwasalimia Watanzania pale sababu ni dakika 60 huwa zinatolewa kuongea na Mfungwa, huwa tunaongea ana kwa ana lakini hatuwezi kupeana hata mikono… tumetenganishwa na kioo hivyo unakaa kwenye upande wako yeye anakaa upande wa pili mnaongea kwa simu ya mezani’

macao 3

‘Nilianza kwenda kutembelea hilo gereza hata kabla Jackie Cliff hajakamatwa, kuna Watanzania waliniona kwenye gazeti la ofisini kwangu ninapofanyia kazi Macao ndio wakanitafuta kuwasaidia, taarifa za Jackie Cliff kukamatwa niliambiwa na Mfanyakazi mwenzangu ambaye huwa ananifanyia make-up’ – Wabogojo

Vipi sasa hivi bado Watanzania wanaendelea kukamatwa kwa dawa za kulevya kwenye mji wa Macao? >>> ‘Naona kesi zimepungua sasa hivi, Wanigeria ndio wamekua wakikamatwa sana…. baada ya kukamatwa Jackie alikamatwa Mtanzania mwingine tu Bwana mdogo alafu baadae akakamatwa Mwanamke mmoja wa Kitanzania baada ya hapo hakuna Mtanzania aliyekamatwa’

Macao
Macao, China

Jackline Cliff aliandika barua kwa Millard Ayo kuwaeleza Watanzania jinsi alivyojutia kwa kitendo alichofanya na kwamba atabadilika baada ya kumaliza kifungo ila hakuweka wazi amehukumiwa miaka mingapi lakini Watanzania wengi waliohukumiwa wamefungwa miaka 6, 8 mpaka kumi kwenye gereza hilo…. bonyeza play kwenye hii video hapa chini kupata barua ya Jackie Cliff.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.