December 2013 ndio zilitoka taarifa rasmi za kukamatwa kwa Mrembo wa Kitanzania Jackie Cliff akiwa na dawa za kulevya kwenye mji wa Macao huko China ambapo alihukumiwa kutumikia miaka kadhaa gerezani.
Jackie alipata umaarufu Tanzania kupitia kuonekana kwenye video kadhaa za bongofleva kama ‘she got a gwan‘ ya Marehemu Ngwea na hata nyingine ya Linex ‘kamugina‘ na baada ya kuripotiwa kukamatwa, kila mmoja akataka kujua kilichotokea na kinachofatia.
Kama sio Jackie Cliff basi inawezekana leo tusingekua tunafahamu ni Watanzania wangapi waliofungwa kwenye gereza moja na yeye kwenye mjia wa Macao… idadi niliyopewa ni 12 ambapo Mtanzania Wabogojo anayeishi na kufanya kazi kwenye mji huohuo wa Macao amesema Wanawake ni wawili tu, Jackie na mwenzie aliyekamatwa karibuni…. huwa anakwenda kuwatembelea Watanzania wote kila Jumamosi.
Wabogojo
amesema ‘kila Jumamosi huwa nakwenda kuwasalimia Watanzania pale sababu
ni dakika 60 huwa zinatolewa kuongea na Mfungwa, huwa tunaongea ana kwa
ana lakini hatuwezi kupeana hata mikono… tumetenganishwa na kioo hivyo
unakaa kwenye upande wako yeye anakaa upande wa pili mnaongea kwa simu
ya mezani’
‘Nilianza kwenda kutembelea hilo gereza hata kabla Jackie Cliff
hajakamatwa, kuna Watanzania waliniona kwenye gazeti la ofisini kwangu
ninapofanyia kazi Macao ndio wakanitafuta kuwasaidia, taarifa za Jackie
Cliff kukamatwa niliambiwa na Mfanyakazi mwenzangu ambaye huwa
ananifanyia make-up’ – Wabogojo
Vipi sasa hivi bado Watanzania wanaendelea kukamatwa kwa dawa za kulevya kwenye mji wa Macao? >>> ‘Naona
kesi zimepungua sasa hivi, Wanigeria ndio wamekua wakikamatwa sana….
baada ya kukamatwa Jackie alikamatwa Mtanzania mwingine tu Bwana mdogo
alafu baadae akakamatwa Mwanamke mmoja wa Kitanzania baada ya hapo hakuna Mtanzania aliyekamatwa’
Jackline Cliff aliandika barua kwa Millard Ayo
kuwaeleza Watanzania jinsi alivyojutia kwa kitendo alichofanya na
kwamba atabadilika baada ya kumaliza kifungo ila hakuweka wazi
amehukumiwa miaka mingapi lakini Watanzania wengi waliohukumiwa
wamefungwa miaka 6, 8 mpaka kumi kwenye gereza hilo…. bonyeza play
kwenye hii video hapa chini kupata barua ya Jackie Cliff.
Note: Only a member of this blog may post a comment.