Akiliachia domo liserereke, Barakah anayebamba na Ngoma ya Siwezi alisema kuwa japokuwa amekuwa akifuatwa na vyombo vingi vya habari kujua ukweli sasa imefika wakati wa kutoa tamko.
“Ujue siku zote nilikuwa sijapata mtu sahihi katika maisha yangu. Nimempata Naj na naamini kwa asilimia zote ana maono ya mbele tofauti na wote niliowahi kuwa nao, pili tunaendana kwa kila kitu na mwisho ni mshauri wangu hivyo sioni sababu ya kuficha,” alisema Barakah.
Note: Only a member of this blog may post a comment.