Sunday, February 28, 2016

Anonymous

Mwanamuziki DIAMOND Platnumz Aamua Kuja Kivingine Sasa Aivamia Fani ya Kurap

Staa wa muziki Diamond Platnumz amejipanga kuachia wimbo mpya wa kurap uitwao Simba.
Akizungumza katika kipindi cha XXL cha Clouds FM Ijumaa hii, Meneja wa msanii huyo, Babu Tale alisema wimbo huo utakuwa sio wa biashara bali ni zawadi kwa mashabiki.
“Kama Hip Hop ni biashara Diamond amefanya wimbo wa kurap lakini hatujauchulia kama ile ni biashara, wimbo umeshaisha na unaitwa Simba,” alisema Babu Tale.
Diamond kwa sasa anafanya poa na video ya wimbo ‘Make Me Sing’ akiwa na AKA wa Afrika Kusini.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.