Wednesday, January 13, 2016

Anonymous

ROSE NDAUKA Amruhusu Rais MAGUFULI Abomoe Tu...!

Rose Ndauka
 Na Gladness Mallya
WAKATI mamia ya wakazi wa Dar es Salaam waishio mabondeni na pembezoni mwa bahari na mito wakihaha nyumba zao kuvunjwa, staa wa filamu Bongo, Rose Ndauka amesema hajali kama nyumba yao itakutwa na bomoabomoa hiyo. 

Badala yake, alimpongeza Rais John Magufuli kwa kusimamia zoezi hilo, kwani wengi wa wanaobomolewa walishapewa taarifa mapema na hawakutii agizo hilo la serikali, lakini akaitaka kuwaangalia kwa jicho la tatu watu ambao hawakupewa taarifa za zoezi hilo. 
 “Wazazi wangu wakibomolewa nyumba naona kawaida tu, siwezi kuwa na presha maana kila kitu kinapangwa na Mungu, kama ni kubomoa wabomoe tu hatuna la kufanya,” alisema Rose.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.