Kundi la vijana hao wakimtembeza Shakila mitaani huku akiwa mtupu.
Na Makongoro Oging’
DUNIA katili!
Mrembo mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Shakila Kocho (21), mkazi wa
Tabata- Kimanga jijini Dar amelazwa Wadi namba 24, Jengo la Mwaisela,
Hospitali ya Taifa Muhimbili kufuatia majeraha yaliyotokana na kupigwa
mawe na kuchomwa moto wa petroli kwa kisa cha tuhuma za kuwa kwenye
mtandao wa wizi wa bodaboda.
Wakimshambulia kwa mawe.
WALIOTEKELEZA UKATILI
Msichana huyo alifanyiwa kitendo hicho
hivi karibuni maeneo ya Buguruni Sukita, Dar na watu wanaodaiwa kuwa ni
madereva wa bodaboda ambao ndiyo waliomtuhumu.
Taarifa zilizopatikana kwa mashuhuda
zinadai kwamba, Shakila kabla ya kuchomwa moto alitembezwa mtupu mtaani
huku watu wakimsonga na baadaye akapigwa mawe na fimbo halafu
akamiminiwa petroli na kulipuliwa kwa kiberiti.
Shakila akiwa ameanguka.
MSOMALI ASAIDIA
Kwa mujibu wa mashuhuda hao, wakati
Shakila akiwa chini kutetea roho yake huku akiungua moto, mwanaume mmoja
mwenye asili ya Kisomali mwenye makazi yake maeneo hayo, alitokea na
kupiga risasi juu kwa lengo la kuutawanya umati na kuwatisha watu hao
kwa mbwa ndiyo ikawa salama ya Shakila.
…Akiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili
BASTOLA YATUMIKA
“Yule Msomali alitoka kwake nadhani ni
baada ya kusikia kelele za auawe…auawe, alipomwona msichana yuko chini
anatapatapa, alitoa bastola akafyatua risasi juu. Watu walikimbia
kidogo, wakarudi, akamfungulia mbwa, ndipo watu wakatawanyika kabisa.
Msomali akawasiliana na polisi Buguruni ambao walikuja kumchukua yule
msichana akiwa ameumia sana na damu zikimtoka, wakamkimbiza Muhimbili,”
kilisema chanzo.
UWAZI MUHIMBILI, MREMBO ATOA SIMULIZI
Ijumaa iliyopita, Uwazi lilimfuatilia
majeruhi huyo Muhimbili ambapo lilimkuta akipatiwa matibabu. Hata hivyo,
baadaye mrembo huyo alipata nafasi ya kusimulia mkasa mzima ulivyokuwa
kama ifuatavyo:
“Nakumbuka ilikuwa mwishoni mwa mwezi wa
kumi (Oktoba) kuja mwezi huu (Novemba). Siku hiyo mimi na mume wangu na
mtoto wetu wa miaka mitatu, tulikuwa bado tumelala nyumbani Tabata
Kimanga, akaja mtu, akabisha hodi. Mimi nikatoka kwenda kufungua mlango.
Ghafla kundi la watu likaingia ndani wakiwa na magongo mikononi,
wakaanza kumshambulia mume wangu bila kusema kisa.
“Kuona vile, mimi nikamchukua mwanangu ili tutoke nje. Wale watu wakakataa mimi kutoka na mtoto, hivyo nikatoka peke yangu. Kule nje nako nikakuta umati wa vijana, baadhi yao walikuwa wamekaa kwenye bodaboda.
“Wengine katika hao vijana niliwatambua.
Walikuwa wamemshika kijana moja ambaye alitobolewa macho na damu
zilikuwa zikimtoka kwa wingi. Mwenye nyumba tuliyopanga akatoka,
alipoona hali ile akaniambia niende kutoa taarifa Kituo cha Polisi
Tabata Shule.”
AKIMBIA, AINGIZWA MTEGONI KWA SIMU
AKIMBIA, AINGIZWA MTEGONI KWA SIMU
“Niliondoka, mbele nikachukua bodaboda
kwa lengo la kwenda polisi. Lakini nikaamua kwenda kwanza Buguruni
Sokoni kwa shemeji yangu (kaka wa mumewe) kumpa taarifa.
“Nilimweleza shemeji hali ya nyumbani
kisha nikamwomba simu yake ili nimpigie mume wangu kujua kinachoendelea
na hali ya mtoto. Lakini simu hiyo ilipokelewa na mtu mwingine
aliyejitambulisha kuwa ni msamaria mwema. Akasema mume wangu ana hali
mbaya kutokana na majeraha ya kipigo, hivyo yupo naye kwenye zahanati
iitwayo Afya Bora iliyopo Vingunguti.
“Mtu huyo alinitaka niende nikaongee na
mume wangu. Nilimuaga shemeji, nikaondoka. Lakini cha ajabu, nilipofika
kule zahanati nikaangukia mikononi mwa wale vijana.”
KILICHOMPATA
KILICHOMPATA
“Walinivamia na kuanza kunipiga huku
wakisema mimi natumiwa na wezi wa bodaboda kama mteja na kuwapeleka
kuuawa na kuporwa bodaboda. Niliwaambia si kweli, lakini hawakusikiliza
utetezi wangu. Walinichukua hadi Buguruni Sukita.
“Kule walinivua nguo zote, nikabaki kama
nilivyozaliwa kisha wakaanza kunitembeza uchi mitaani. Kwa kweli
walinifanyia mambo ya kunidhalilisha sana kiasi kwamba mengine nashindwa
kuyatamka.”
APIGWA KWA MAGONGO, MAWE NA MATOFALI
APIGWA KWA MAGONGO, MAWE NA MATOFALI
“Kunitembeza bila nguo hakukuwatosha,
wakaanza kunipiga kwa magongo, mawe na matofali. Niliishiwa nguvu mpaka
nikadondoka chini huku nikitokwa na damu nyingi. Bado wakaona haitoshi,
wakaona wanimalizie kabisa, wakanimiminia petroli na kunilipua kwa
kiberiti huku nikishuhudia ila sikuwa na nguvu ya kujinasua.
“Kule Sukita nilikuta watu wengine
wawili wakiteketea kwa moto mpaka wakafariki dunia. Nimeambiwa katika
watu wale, kumbe mmoja ni mume wangu.”
AMTAJA MSOMALI
AMTAJA MSOMALI
“Ni Msomali mmoja ndiye aliyepita maeneo
yale na kunizima moto kisha akapiga simu polisi. Sikujua
kilichoendelea. Nilijitambua nikiwa hapa hospitali, nikaambiwa ni
Muhimbili.”
AMZUNGUMZIA MTOTO WAKE
AMZUNGUMZIA MTOTO WAKE
“Mpaka sasa sijui mtoto wangu yupo wapi.
Na kama yupo nyumbani, yupo na nani!? Nakumbuka yeye alianza kulia
mara tu alipomwona baba yake anasulubiwa kwa magongo.”
WITO WAKE KWA JESHI LA POLISI
WITO WAKE KWA JESHI LA POLISI
“Naliomba jeshi la polisi kuwatafuta na kuwakamata wale wote waliohusika kunifanyia mimi unyama huu na kumuua mume wangu.”
WALIVYOSEMA WAENDESHA BODABODA
WALIVYOSEMA WAENDESHA BODABODA
Uwazi lilipata nafasi
ya kuzungumza na baadhi ya waendesha bodaboda wa maeneo ya Buguruni
ambao walisema Shakila alituhumiwa kuwa mhusika mkuu anayetumiwa na wezi
kukodisha usafiri huo kwenda eneo walipo wezi hao kisha kuporwa fedha
na bodaboda, wakati mwingine hadi kuuawa.
Waliendelea kudai kuwa, mrembo huyo
alishajulikana na watu wa bodaboda kwamba akikodisha pikipiki hairudi
wala dereva kuonekana na wengine maiti zao kuokotwa mbali zikiwa na
majeraha.
KAULI ZA WANANCHI
KAULI ZA WANANCHI
Baadhi ya wananchi walikilaani kitendo
hicho cha kujichukulia sheria mkononi bila kuwafikisha watuhumiwa katika
vyombo vya dola na wameitaka polisi kuwatafuta wahusika wote na
wachukuliwe hatua za kisheria.
BAADHI YA WATUHUMIWA WADAKWA
BAADHI YA WATUHUMIWA WADAKWA
Hata hivyo, habari kutoka Kituo cha
Polisi Buguruni, Dar zinasema kuwa, vijana kadhaa wanaodaiwa kuhusika na
tukio hilo wamekamatwa na bado polisi wanaendelea kuwatafuta wengine
ili sheria ichukue mkondo wake.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, SACP Lucas Mkondya alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na watuhumiwa saba wanashikiliwa.

Note: Only a member of this blog may post a comment.