Gladness Mallya
Aliyekuwa mke wa Emmanuel Mbasha, Flora Mbasha
Emmanuel Mbasha na mkewe
MWIMBAJI wa nyimbo za Injili na 
mfanyabiashara maarufu Bongo, Emmanuel Mbasha amepotezea kuzungumzia 
suala la kumpa talaka mkewe kwa madai kwamba yupo bize na suala la 
sherehe za ushindi wa rais Dk. John Pombe Joseph Magufuli.
Mbasha aliitoa kauli hiyo hivi karibuni 
wakati mwanahabari wetu alipomuuliza mwimbaji huyo kuhusu hatma ya kutoa
 talaka ambayo aliyekuwa mkewe, mwimbaji Flora Mbasha amekuwa akiidai 
hadi kumfikisha mahakamani.
“Sikia bwana, mimi kwa sasa nipo bize na
 sherehe za ushindi wa Magufuli siwezi kupoteza muda wangu kuzungumzia 
vitu vidogovidogo kama hivyo, kwangu mimi rais wa nchi ni muhimu kuliko 
hayo mambo ya Flora unayoniulizia,” alisema Mbasha.
Emmanuel na Flora walikuwa wanandoa na 
kubarikiwa kupata mtoto mmoja kisha kugombana na kufikia hatua ya 
kuachana na sasa kila mmoja anaishi kivyake.

Note: Only a member of this blog may post a comment.