Sunday, November 22, 2015

Anonymous

Good News: Neema Jijini Dar Mwezi Ujao

Mradi wa mabasi yaendayo hataka DART unatarajia kuanza kutoa huduma ya usafiri mwezi ujao jijini Dar es salaam.
Meneja miundombinu wa DART Mohamed Kuganda amesema ujenzi wa miundombinu ya mradi umekwenda vizuri na kusisitiza katika ya mwezi ujao huduma zitaanza kufanya kazi.

“Ujenzi wa miundombinu umefikia pazuri, wahusika wanakimbizana na muda kukamilisha sehemu zilizobakia”.

Alisema barabara za mradi ambazo zimefumuliwa kutokana na wakala wa usimamiaji TANROADS kutoridhishwa na baadhi ya sehemu za barabara hizo na kuongeza kuwa ufumuaji wake hautaathiri mipango ya mradi.
Alisema mradi huo utafanikiwa kama ulivyopangwa endapo wadau watatimiza majukumu yao ya ndani ya muda waliojiwekea.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.