
Meneja miundombinu wa DART Mohamed Kuganda amesema ujenzi wa miundombinu ya mradi umekwenda vizuri na kusisitiza katika ya mwezi ujao huduma zitaanza kufanya kazi.
“Ujenzi wa miundombinu umefikia pazuri, wahusika wanakimbizana na muda kukamilisha sehemu zilizobakia”.
Alisema barabara za mradi ambazo zimefumuliwa kutokana na wakala wa usimamiaji TANROADS kutoridhishwa na baadhi ya sehemu za barabara hizo na kuongeza kuwa ufumuaji wake hautaathiri mipango ya mradi.
Alisema mradi huo utafanikiwa kama ulivyopangwa endapo wadau watatimiza majukumu yao ya ndani ya muda waliojiwekea.
Note: Only a member of this blog may post a comment.