CHEZEA kifo wewe! Mwalimu wa Shule ya Msingi Mwere
ya mjini hapa ambaye jina halikupatikana mara moja, akiwa mjamzito,
amenusurika kifo baada ya daladala walilopanda kutumbukia mtaroni na
yeye kuchomokea kwenye dirishani.
Gari likiwa limepinduka baada ya ajali hiyo.
Tukio hilo lilijiri jirani kabisa na eneo la Kanisa la KKKT ambapo
mashuhuda walidai kwamba tukio hilo lilitokea baada ya dereva wa
daladala aliyefahamika kwa jina moja la Mathias kumuachia ‘deiwaka’
kijana mwingine aliyetajwa kwa jina la Arird Tito.
Mashuhuda wakiwa eneo la tukio.
....Mmoja wa shuhuda akielezea jinsi ajali hiyo ilivyotokea.
Baada ya dereva wa gari kubwa kuona hivyo hakumpa nafasi dereva huyo
ndipo akajikuta anatumbukia mtaroni.“Baada ya gari kutumbukia mtaroni,
ticha huyo na madenti wake walilazimika kuokoa maisha yao kwa kutokea
kwenye madirisha ya daladala hiyo,’’ alisema Tito ambaye alikuwa ni
kondakta wa daladala hiyo.Hata hivyo, abiria hao hawakuumia sana zaidi ya kupata michubuko ya hapa na pale, kabla ya kupelekwa hospitalini kwa matibabu.
Note: Only a member of this blog may post a comment.