Wednesday, October 14, 2015

Anonymous

WAGOMBEA WOTE WANAOTUMIA LUGHA ZA MATUSI, VITISHO KUKIONA CHA MTEMAKUNI!

Mtwara. Polisi mkoani Mtwara imewaonya wagombea na wafuasi wao kutumia lugha za matusi, vitisho pamoja na fujo katika mikutano ya kampeni.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Henry Mwaibambe alisema hayo jana na kuongeza kuwa hali hiyo inaweza kuchochea uvunjifu wa amani.


Alisema wagombea hao wamekuwa wakikiuka taratibu na sheria za nchi wakati wakifanya kampeni.
“Nawakumbusha wagombea na wafuasi wao kwamba kabla ya kampeni kuanza vyama vya siasa vilisaini vitabu vya maadili ya uchaguzi.
“Na kwamba hawaruhusiwi kufanya mambo ambayo hayapo kisheria, atakayekiuka ataadhibiwa,” alisema Kamanda Mwaibambe.
Kamanda alisema wagombea wa vyama hivyo hawaruhusiwi kubeba sanamu, vinyago au kutumia kitu chochote kitakachoonyesha kinafanya udhalilishaji wa chama kingine katika mikutano yao ya kisiasa.

Pia, alisema wagombea na wafuasi wao hawaruhusiwi kutumia vipaza sauti kuanzia saa 12 jioni ili kuepuka kukiuka taratibu na maadili ya uchaguzi.
Hata hivyo, Kamanda Mwaibambe alisema kuanzia sasa polisi hawatamvumilia mtu atakayevunja taratibu na sheria katika kipindi kifupi kilichobaki cha kampeni hadi itakapofikia siku ya uchaguzi.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.