Magufuli akimwaga sera katika Viwanja vya TP TP Sinza.
Mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk John
Pombe Magufuli leo ametoka jijini Mwanza kuingia jijini Dar es Salaam
kwa ajili ya kampeni za lala salama kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika
jumapili hii.
Akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Mwl julius Nyerere, Magufuli alikutana na kusalimiana na
rais Jakaya Mrisho Kikwete aliyekuwa akisafiri kutoka Dar es Salaam
kuelekea mkoani Ruvuma kuwaaga wananchi wa mkoa huo.
Baada ya hapo Magufuli aliendelea na
ratiba yake ya mikutano ya kuomba ridhaa kwa wakazi wa Dar es Salaam.
Maeneo amabyo magufuli amefanya mkampeni leo ni pamoja na Kigamboni
katika Uwanja wa Machava, Mbagala Zakhiem, Ubungo Bus Terminal, Ubungo
Shekilango, Tandika Mwembeyanga, Uwanja wa TP Sinza na kumalizia
mkutano mkubwa katika viwanja vya Biafra.
Akiwahutubia wananchi wa Kigamboni,
Magufuli aliwatoa hofu kuwa hakuna atakayedhurumiwa kufuatia ujenzi wa
mjiwa kisasa katika eneo hilo. pia alisema eneo hilo atalifanya kuwa
wilaya mpya ili liwe na hadhi na kupewa huduma zote kama jimbo
linalojitawala. Baada ya kuwa wilaya ataipatia Hospitali ya Wilaya na
huduma zingine zitaongezwa.
Akiwa maeneo mengine, Magufuli aliwanadi
wabunge na madiwani wanaowania nafasi hizo kwa tiketi ya CCMhuku
akiwaahidi wananchi kuwaboreshea maisha, kupambana na rushwa na
mafisadi.
Pia aliongeza kuwa, daraja la Kigamboni linatarajiwa kukamilika mwezi ujao ambapo wananchi watavuka bure.
PICHA NA RICHARD BUKOS/GPL

Note: Only a member of this blog may post a comment.